NASREDDINE
 Nabi, Kocha Mkuu wa Yanga ameweka wazi kwamba hakuna mchezaji mkubwa 
ndani ya kikosi cha Yanga kwa kuwa Yanga ni kubwa kuliko yoyote.
Kocha huyo 
raia wa Tunissia ameongeza kuwa kuhusu kuanza kikosi cha kwanza kwa 
wachezaji wake itategemea na namna hali itakavyokuwa kutokana na mchezo 
husika na haina maana kwamba kufunga mabao ni sababu ya kuweza kuanza 
kikosi cha kwanza.
Ikumbukwe 
kwamba nyota wake Heritier Makambo kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho 
dhidi ya Ihefu FC uliochezwa Uwanja wa Mkapa aliweza kufunga mabao 
matatu lakini Nabi amebainisha kwamba hawezi kuwa na uhakika wa kuanza 
kikosi cha kwanza.
“Kila 
mchezaji ndani ya Yanga ni muhimu na ipo wazi kwamba Yanga ni kubwa 
kuliko mchezaji hivyo haina maana kwamba kufunga ama kutofunga ni sababu
 za mchezaji kuanza kikosi cha kwanza.
 
“Ninafurahishwa
 na uwezo wa wachezaji wangu wote kila mmoja anatimiza majukumu yake 
kuhusu kuanza ama kutokuanza kikosi cha kwanza wote wanastahili kucheza 
na inategemea na mbinu ya mchezo husika,”amesema.